KCSE Past Papers 2017 Kiswahili Paper 3 (102/3)

Kenya Certificate of Secondary Education

2017 Fasihi Karatasi ya 3

Sehemu A: Fasihi Simulizi

Lazima (20 marks)

Sama utungo ufuatao kisha ujibu maswali.

Walikuja mahasidi, ah, walikuja

Nyayo zao zikirindima, ah rindima

Kwa ghamidha ya uadui, 00 uadui

Wali Wakibeba sime

Wali wakibeba mata

Wali Wakibeba mienge

ya moto kutangazia

kwao kuwasili

Walikuja kwa ndimi

zilohimili cheche

matusi kutumwaiya.

Hawakuj ua ya kwamba

mbele ya mhimili huno wetu

wao wali vipora.

Kwenye Mlima wa Sugu, walituvamia.

Aliwakabili Mbwene

Mwana wa Ngwamba, ee Mbwene

Aliwakabili Mbwene kwa kitali kikali.

Wali wametuteka ja samaki kwenye dema

Wali wamewapukutisha

wetu mabarobaro

Aliwakabili Mbwene

Ee Mbwene, Mwana Wa Ngwamba

Aliwakabili

kwa hamasa za ujana

kwa uchungu wa kuumbuliwa

wa wetu wana.

Aliwakabili Mbwene

Nao wakalipiza shambulizi

kwa kujidai majagina

walijibwaga uwanjani

Laiti wangalijua wanajikabidhi

viganjani mwa Mbwene.

Aliwakabili Mbwene, ee

Mwana wa Ngwamba, shujaa asoshindwa

alipigana kitali

cha kufa na kupona

kuiopoa jamii yetu,

kuirejesha hadhi yetu.

kuirejesha mifugo yetu

kuwarejeshea wakulima vikataa vyao

kuwaokoa vipusa wetu

nyara Waliotekwa, ati Walipiza kisasi.

Aliwakabili Mwana Wa Ngwamba

Aliwakabili Upepo Wa Kusi

Hata kikorno cha mapambano kilipofika

Wagundi walijua kwamba

Walikuwa na Mwana, ee Mwana

Mbwene, ee Mwana wa Ngwamba Hakuwa na kifani, ee kifani

Alipigana nao, cc Mwana wa N gwamba

Kwa siku kumi bila tonge wala tone la maji

Kwetu kukenda kicheko cha Wokovu

Kwao kukenda kilio.

(a) “Huu ni wimbo wa sifa.” Thibitisha kauli hii kwa kutoa mifano mitatu kutoka kwenye utungo huu. (alama 3)

(b) Andika sifa tatu za jamii ya nafsineni katika utungo huu. (alama 3)

(c) Huku ukitoa mifano, bainisha vipengele vinane vya kimtindo ambapo nafsineni imetumiwa kufanikisha uwasilishaji wa umngo huu. (alama 8)

(d) Tungo za aina hii zinaendelea kufifia katika jamii yako. Fafanua hoja sita utakazotumia kuishawishi jamii yako kukinga dhidi ya hali hii. (alama 6)

SEHEMU B: RIWAYA K. Walibora: Kidagaa Kimemwozea Jibu swali la 2 au la 3.

2. “Lakjni waliogopamwaliogopa hata kuwa na uoga.”

(a) Eleza muktadha wa dondoo hili. (alama 4)

(b) Bainisha tamathali lnoja ya usemi ambayo imetumiwa katika dondoo hili. (alama 2)

(c) Kwa kurejelea hoja kumi na nne kutoka kwenye riwaya hii, thibitisha kwamba raia wa Tornoko walistahili kuogopa hata kuwa na uoga‘ (alama 14)

3. (a) “Usinivue nguo kwa macho yako wee!”

Kwa kurejelea hoja kumi na mbili kutoka kwenyc riwaya hii, thibitisha kwamba mzungumzaji anastahili kuvuliwa nguo. (alama 12)

(b) Tathmini umuhimu wa barua ya Ben Bella kwa Mashaka katika kuijenga riwaya hii. (alama 8)

SEHEMU C: TAMTHILIA T. Arege: Mstahiki Meya Jibu swali la 4 au la 5.

4. “Tuyashughulikie ya leo. Kesho, keshokutwa na mtondo harutakuwepo. Wayatakig nigi ya mtongggoo? ”

(a) Eleza muktadha wa dondoo hili. (alama 4)

(b) Bainisha sifa ya rnzungumzaji inayodokezwa na kauli iliyopigiwa mstari. (alama 1)

(c) Eleza sifa tano Za anayeambiwa maneno haya. (alama 5)

(d) Kwa kurejelea hoja kumi kutoka kwenye tamthilia, onyesha jillsi kutoyataka ya mtondogoo kulivyozorotesha hali ya maisha Cheneo. (alama 10)

5. “Ni mgao Wa wakubwa kula kwanza na sisi wengine kupigania makombo yanayoanguka chini.” (a) Fafanua sifa tano za rnzungumzaji. (alama 5)

(b) Thibitisha ukweli wa kauli hii kwa kurejelea hoja kumi na tano kutoka kwenye tamthilia. (alama 15)

SEHEMU D: USHAIRI

Jibu swali la 6 au la 7.

6. Soma shairi lzfuatalo kisha ujibu maswali.

Mwanangu, Wenye dhambi vishawishi, vikejeli

Mwanangu, katu wasikushawishi, binkuli

Mwanangu, aushi nayo uishi, kama mwali

Mwanangu sikubali!

Mwanangu, sherati sikuperembc, kakubali

Mwanangu, usiwache wakubembe, kwa sali,

Mwanangu, mithili yao mapembe, ya fahali

Mwanangu sikubali!

Mwanangu, wajeuri siwe nao, ni shubili

Mwanangu usifwate njia zao, pita mbali

Mwanangu, ujeuri scra yao, mazohali,

Mwanangu sikubali!

Mwanangu, Waongo usiwasifu, kulihali

Mwanangu, uongo ubatilifu, si amali

Mwanangu, ndimi zao hazikifu, si manzili

Mwanangu sikubali!

Mwanangu, wafisadi siwe nao, kemikali

Mwanangu, tamaa ndo utu wao, si Injili

Mwanangu, Wahepe kila uchao, kiakili

Mwanangu sikubali!

Mwanangu, wote walio wabaya, Wanadhili

Mwanangu, usije ukawapeya, ikibali

Mwanangu, katika hino duniya, kaa mbali

Mwanangu sikubali!

(J. Kiponda)

( a) Fafanua mambo sita ambayo yanaweza kuzorotesha maadili ya anayelengwa na shairi hili.

(b) Bainisha tamathali mbili za usemi zilizotumiwa katika shairi hili.

(c) Andika aina mbili za urudiaji zilizotumiwa katika shain’ hili.

(d) Ainisha shairi hili kwa kuzingatia vigezo vifuatavyoz

(i) idadi ya vipande katika mishororo.

(ii) mpangilio wa maneno katika mishororo

(m) idadi ya mizani katika mishororo.

(iv) mpangilio wa vina katika beti.

(e) Andika aina mbili za uhuru wa kishairi zilizotumiwa katika shairi hili.

if I Andika ubeti wa tano kwa lugha ya nathari.

Soma Shairi Iifizatalo kisha ujibu maswali.

Walo nacho hawachi mshangao kunitia Moyoni watakutia pindi waonapo we u chambo cha kuvutia rasilimali huko kwenye vina Hawachi kukwinamisha kukupindisha mgongo ndoana urneshika kuvulia yao riziki. Watakwita kwa majina ya hadhi ya kupembeja ya kukwaminisha kwamba We na wao mu

Wamoja hali zenu kama sahani na kawa wanakwonyesha wao nawe mwachumia jungu moja yenu matarajio ni mamoja Watakwahidi halua kila tunu watakwashiria

mradi nyoyo zao zimemaizi We u nundu ya kukamulia mafuta we u ndovu wa mti kugonga makoma kuangusha wafaidi wao. Mabepari wana mambo ukiwa yao makasia ya kuliendesha dau lao majini lielee miamba kulepusha Watakusifil Watakuchajiisha mbele utunge machoyo yenye ari huku wanakufunga nira ja fahali

mali kuwazalishia huku kipato wakupimia kwa kibaba usipate kukidhi haja usipate kujarnini kuwategemea uzidi. Hawa ni wa kuajabiwa

Watakupa yao kazi Mpangilio wa kazi wakukabidhi Wao na malengo wakupe La! Hawakupi! Wanakuhusisha katika kuyavyaza na muda wa kuyafikia nao mwaafikiana ati kuna makubaliano bayana ambayo ubatizo Wayo ni kandarasi ya utcndakazi. Ela We nao mnajua ndo kigezo cha kupimiamWako uwaj ibikaji

wako mchango chunguni yako thamani Na usidhani una hiari ya kuamua tapofika Watakusukuma lmfikia yao shabaha bila lmwazia ujixa wanokupa. Watakuhimiza kuturnia chako kipawa kuikoza nundu yao mafuta Viumbe hawa! Mabepari – waajiri

(a) Eleza mikakati sita inayotumiwa na waajiri kujikuza kiuchumi. (alama 6)

(b) Bainisha tamathali tatu za usemi zilizoturniwa katika shairi hili. (alama 3)

(c) Huku ukitoa mifano, bainisha aina mbili za uhum wa kishairi aliotumia mshairi.

(d) Andika mifano ya mistari mishata katika shairi hili.

(6) Bainisha nafsineni katika shairi hili.

(f) Fafanua toni ya shairi hili.

(g) Andika ubeti wa tatu kwa lugha ya nathari.

SEHEMU E: HADITH FUPI K. Walibora na S. A. Mohamed (Wah): Damu Mveusi na Hadithi Nyingine

8. (a) Tathmini urnuhimu wa Lucy katika kuijenga hadithi, “Tazamana na mauti”

“Mizizi ya Matawi” (Ali A. Ali)

(b) “Aaa, bibi yangu namuomba Mungu anisamehe dhambi zangu ..”’

(i) Eleza muktadha Wa dondoo hili.

(ii) “Jamii ya,” Mizizi ya Matawi azamana na Mauti.”atawi inastahili kusamehewa ” Fafanua kwa kutoa hoja sita kutoka kwenye hadithi.

(Visited 298 times, 1 visits today)
Share this:

Written by