KCSE Past Papers 2020 Kiswahili Karatasi ya 3 (102/3)

Karatasi Ya 3

Mwongozo Wa Kusahihisha

i. Mzungumzaji ni Mwalimu Mstaafu

ii. Anazungumza na hadhira ambayo imekukja kumuaga

iii. Yuko shuleni

II. Toni ya kuonya/kutahadharisha – si vizuri kukitia kutumbua mchanga

III.

i. Kuwadhalilisha wenzake kama vile Baraka, FEsto, Mshamba na Nangeto

anapoonyesha hali yao mbaya ya awali

ii. Kufichua njama za kifisadi- anasema pesa zilizochangishwa na rais zililiwa na

wakora kama vile akina Festo

iii. Anapewa nafasi yka Mwalimu Mosi kuhutubu lakini anamuaibisha anasema

anafurahia kuondoka kwa Mwalimu Mosi

iv. Kutotambua mchango wa Mwalimu Mosi – anasema Mosi ataondoka shule ipumzike

v. Anashindwa kustahimili changamoto shuleni

vi. Anajidhalilisha kwa kusifia suala kama vile utapeli na wizi, hajiamini – anajiita

zumbukuku asiyeweza kuimarika

vii. Anakosa kuyawajibikia maisha yake. Anamlaumu Mwalimu Mosi, anasema

umaskini wake ulisababishwa na Mwalimu Mstaafu

2

viii. Anakosa kuwajibikia Familia yake. Hatekelezi majukumu yake kama mume na

mzazi

ix. Kutelekeza familia – hakuwahi kupita kwa Mwalimu Mosi kuwajulia hali

wanafamilia yake (uk. 128)

x. Kukmhuribia Mwalimu jina kwa kusema kuwa amekioa kitoto chake (uk. 130)

b).i. Taswira – uoni – nyeupe, nyembamba

ii. TAshihisi – vi kujianika

iii. Takiriri uridiaji – Alijaaliwa mvi

iv. Tashbihi – kama theluji

v. Taashi – mvi – ishara ya hekima

vi. Kinaya

vii. Usimulizi

viii. Chuku /Udumisi

ix. Mdokezo

2. a) i. Haya ni maneno ya msimulizi

ii. Yanamhusu Sauna

iii. Sauna yumo nyumbani mwa Bi. Kangara

iv. Anahisi anakabiliwa na hatari Fulani ndipo moyo unamwenda mbio

v. Anapofungua lango anakumbana na polisi ana kwa ana.

II

i. Taswira hizi – anahisi/kikali

ii. Mwendo – anatoka nje, moyo kumwenda mbio, kusimama

iii. Usikivu – mbisho hafifu/anasikia

iv. Mguso – vipapasio

III

i. Tasbihi – anajihisi kama anayetarajia kuwa na kinyang’anyiro cha upiganaji

masumbwi

ii. Tashhisi – kusimama kwa vipapasio vya akili/moyo wake ukimwambia

iii. Mdokezo wa methali – yake ya arobaini imefika

iv. Kutumia usimulizi wa wakati uliopo – mara anasikia

v. Nahau – kumwenda mbio

b)3i. Kunyesha changamoto zinazokumba hospitali za umma. Selume anashangaa namna

alivyoweza kustahili matatizo kama vile ukosefu wa glavu hospitalini.

ii. Kuangazia suala la ufisadi. Dawa zilizotengewa hospitali zinauzwa na wasimamizi

wa hospitali (uk. 140). Ruzuku kutolewa kwa wasiostahili.

iii. Kuonyesha ukosefu wa uwajibikaji wa wasimamizi wa taasisi za umma. Hospitali

haijalipia umeme (uk. 140)

iv. Kuendeleza ploti – kupitia sadfa. Kituo kinakamilika wakati ambapo Sulume

anajiuzulu; anapata kazi na mkondo wa matukio kubadilika

v. Kuonyesha migogoro inayosababishwa na tama ya rasimlimali. Mgonjwa

analemazwa katika mapigano ya kung’ang’ania ardhi (141)

vi. Kujenga tabia za wahusika. Kwa mfano, utu wa Ridhaa. Anaanzisha kituo cha afya

na kuwapa ajira Selume na Kaizari

vii. Kuonyesha athari za matumizi mabaya ya vileo. Mwanafunzi anakufa kutokana na

pombe harame (uk 142).

viii. Kuonyesha ukengeushi. Wasomi wanashindwa kukabiliana na matatizo/changamoto

wanatumia mbinu hasi ili kujisahaulisha na hali yao duni (uk. 142)

ix. Kuangazia changamoto zinazokumba sekta ya elimu. Halmashauri ya mikopo

kutotosheleza mahitaji ya wanafunzi

x. Kuonyesha umuhimu wa mshikamano a kifamilia katika maisha ya watoto. Kipanga

anaingilia matumizi mabaya ya vileo kwa kukataliwa na aliyedhani ndiye babake.

xi. Kuonyesha athari za kufuata mila zinazorudihsa nyuma maendseleo ya kijamii.

Tuama anakasirika kwa kupashwa tohara

xii. Kuaangazia suala la ukiukaji wa haki wa zatoto. mama yake Pete kutoshughulika

kutambua kwamba binti yake amekua na mahitaji yake yamebadilika

xiii. Kuonyesha jukumu la ujamii katika kuwarithisha vijana mbinuishi. Mwanzo mpya

inawapa vijana kama vile kipanga huduma za ushauri nasaha unaoshaidia kubadilisha

tabia

xiv. Kuangazia uozo wa kijamii. Uavyaji mimba – Pete anajaribu uavya mimba.

3. a)i. Nahau – Kujitanua kifua

ii. Mdokezo wa methali – mimi ni mwana wa mhunzi na bila shaka wa mhunzi

asiposana huvuvia

iii. Chuku – kuinua tani mia moja/kufufua maiti

iv. Tashbihi/ulinganishi – kama Yule mbabe wa kivita

v. Bilagha – angeweza kuinua tani ngapi vile za chuma?

vi. Taswira – uoni – kuinua, wakitazama

vii. Mbinu rejeshi – hadithi ya Fumo Liyongo na ile ya Akavi

viii. Tabaini si tofauti

ix. Udokezaji – anadokeza ushujaa wa Liyongo hatujui ni shujaa wa aina gani

4 x. Ubanaji – Baba, babangu

xi. Utata – matumizi ya neon hivi yanaweza kurejelea dhana zifuatazo

a) Namna

b) Kimchezo

c) Bila kusumbuka

d) Palepale

e) Wakishangaa

xii. Kutumia usemi halisi na wa taarifa

b).i. Kuendeleza mshikamano/ushirikiano wa kifamilia. Mwangeka na Mwangemi

wanapendana. Wanashiriki shughuli mbalimbali

ii. Kuangazia historia ya jamii. Mwangeka anataja vita baina ya jamii yake na Akavi ili

kuwaokoa mifugo. Kutajwa kwa mashujaa

iii. Kuendeleza tamaduni kama vile utambaji. Nyanya anawahadithia kina Mwangeka

kuhusu Fumo Liyongo

iv. Usuluhishaji migogoro/kuendeleza shughuli za usuhilishaji wa migogoro katika

jkamii. Babu Msubili ni jaji wa kienyeji

v. Kudhibiti vitendo vya wanajamii/kupitisha na kuendeleza imani za kijamii. Babu

hakupenda kukutana na mwanamke asubuhi. Mama ya msimulizi anawakataza

kumpelekea uji asubuhi; anawatuma ndugu wake wa kiume

vi. Kudumisha nidhamu. Mwangeka na Mwangemi wanapomwiga Babu wanachapwa

na Babu, kasha wanakatazwa chakula.

vii. Kutoa mwongozo kuhusu namna ya kushi. Mama mwangeka na Mama Mwangemi

wanakilaani kitendo cha kukmwiga babu; wanawaadhibu zaidi ili kukomesha tabia

hii.

viii. Kudumisha mahusiano ya kijamii/kaida zinazoongoza mahusiano ya kifamilia.

Mwangeka na Mwangemi wanamwiga Babu ili kumkumbusha kwamba anastahili

kuwa mtani wao kama ilivyo desturi ya jamii yao

ix. Kuendeleza shughuli za kijamii, kwa mfano michezo ya watoto na uigizaji

x. Kendeleza imani kuhusu majukumu ya jijinsia katika jamii. Mwangeka anapobeza

kuwepo kwa shujaa wa kike (Mekatilili uk 179). Kuonyesha imani ya jamii kwamba

shujaa wa kivita sharti awe mwanaume. Babu anamkumbusha mwangeka kuwa

wanaume hawalali mapema

xi. Kuendeleza mbinu za kijadi za urekebishaji tabia/ufunzxaji wa maadili. Babu

anatumia kichapo, ambacho njia pekee iliyoaminika kumshinikiza motto kutii

xii. Kuhimiza maridhiano. Mwangeka na mwangemi wanawapa majogoo wao punje za

mahindi pamoja na kuwakumbusha asiyekubali kushindwa si mshindani (uk. 183).

5

4. a).i. Ni maneno ya Aisya/Mamapima

ii. Anawaambia wanasaagamoyo walikutana sokoni

iii. Wapo kwenye lango kuu sokoni

iv. Pombe yake imemwagwa; anajutia matendo yake ya awali

b) . i. Usambamba – Nilijua ninawaponza

Nilijua ninawapunja

ii. Tashhisi – Nilimezwa na tama

c). Ploti

i. Kupitia kwake tunaelezwa kuhusu usuli wa utoaji wa kandarasi ya uokaji keki; yna

Ngurumo walimwandama Husda

ii. Baadhi ya matukio katika maisha ya wahusika Fulani yanaangaziwa katika kibanda chake

cha pombe. Ngurumo anasema alisoma na Tunu (uk. 57). Tunaonyeshwa kuwa Siti

alikuwa mlevi hapo awali (uk. 58).

iii. Wimbo anaimba Mamapima ni kipengele cha ploti. Anautumia kuitetea kazi yake (uk

60.)iv. Anajenga mgogoro kati ya wanamabadiliko na wanaotaka hali ibakie hivyo. Tunu

anasema amekuja kuwakomboa walevi ilhali Mamapima anasema anaharibiwa biashara.

v. Matukio kwenye biahsara yake yanawezesha kujua nani aliyempiga na kumuumiza Tunu.

Ngurumo anaashiria miguu ya tunu iliyoumia (uk. 63)

vi. Kuonyesha hatima ya mgogoro baina ya viongozi na wanyonge. Anasema wamemgeuka,

wameimwaga pomebe

vii. Kuonyesha mustakabali wa Sagamoyo. Anajuta, anaomba msamaha; anaonyesha

kuibadili nia/kueleza uaminifu ake kwa Tunu; anataka kuibusu miguu ya Tunu (uk. 92).

Maudhui

i. .Anaendeleza suala la ufisadi. Anapewewa kandarasi ya kuoka keki kwa kuwa yeye ni

rafiki kya Husda

ii. Kuonyesha upujufu wa maadili. Anahusiana na Ngurumo kimapenzi

iii. Kuonyesha ukosefu wa uwajibikaji. Anauza pombe haramu huku akijua ni hatari

iv. Anaangamiza kizazi cha cijana. Kwa kuwauzia dwa za kulevya (mtu I, mtu ii

wameathirika na matumizi ya dawa za kulevya) (uk. 62)

v. Anaonyehsa matumizi mabaya ya cheo. Anapewa kibali cha kuuza pombe haramu kwa

sababu mumewe ni kikaragosi cha watawala

vi. Anaonyesha haja ya maridhiano. Anajutia matendo yake, anaomba masamaha na

kumtambua tunu (anataka kumbusu)

6vii. Kuangazia mabadiliko. Anajutia aliyotenda. Anajiunga na wanaotetea mabadiliko

viii. Anaendeleza maudhui ya tama na ubinafsi. Anauza pombe haramu bila kujali athari zake

kwa jamii. Kumweka Husda kawpani ili anufaike.

5. a)i. Wanachangia kuendeleza uchumi. Hata wanapokosa ajira, wanajiajiri. Sudi anachonga

vinyago; Ashua anauza mandazi

ii. Wanapigania haki za wanyonge. Tunu na Sudi wakiwa chuoni walikuwa viongozi wa

harakati za kupigania haki

iii. Wanawazindua wanasagamoyo kuhusu haja ya kuwa na uongozi unaozingatia misingi ya

kidemokrasia. Tunu na Sudi wanawahamasisha Wanasagamoyo kuhusu aki zao

iv. Wanaukosoa uongozi. Tunu anamkabili Majoka na kumwambia kwamba

Wanasagomoyo wana haki ya kuihsi (uk. 45)

v. Wanahimiza haja yka kuzingatia maadili ya kijamii. Ashua anaheshimu asasi ya ndoa.

Anakataa ushawishi wa Majoka

vi. Wanachangia kuboresha hali ya utendakazi katika taaluma zao. WAlimu wanagoma ili

kupata mazingira mazuri ya kufanyia kazi

vii. Wanatoa kielelezo cha uongozi ufaao. Tunu anasema kwamba wanahitaji viongozi

wanaofahamu matatizo yao

viii. Wanafunza kuhusu umuhimu wa familia na malezi. Sudi anamwambia Ashua awafikirie

watoto wao (uk. 48)

ix. Wanaunda na kuimarisha itikadi za kijinsia zinazowawezesha kuleta mabadiliko katika

jamii. Licha ya Sudi na Tunu kushukiwa kuwa wapenzi, hawalegezi juhudi zao za

kuuhamasisha umma. Sudi anachonga kinyogo cha mwanamke.

x. Kuwakosoa wanyonge ambao wanatumiwa kama vibaraka. Tunu anamuuliza Ngurumo

kipi muhimu; dhifa au kufunguliwa kwa soko. Sudi anawatanabahisha kina Boza kuhusu

suala la mijikata

xi. Baadhi yao wanaendeleza ubaguzi wa kijinsia. Ngurumo anasema hawezi kumpa

mwanamke kura.

xii. Wanasisitiza umuhimu wa elimu na ustaarabu. Ashua anasema kutoelemika kuna tatizo

(uk. 28), naye Husda anasema elimu bila ustaarabu haifai

xiii. Baadhi wanakwamiza juhudi za kupigania haki. Ngurumo anatumiwa na Majoka

kumpiga na kumnyamazisha Tunu.

b).i. Kuendeleza mgogoro wa kinafsia. Majoka anasema kuna kilio kikubwa ndani kwa ndani

(uk. 73).

ii. Kuchumuza matukio ya awali; kwa mfano kuuawa kwa Jabali (uk. 73)

iii. Kudokeza hatari iliyomnyojea Majoka – mikono yangu imefungwa kwa minyororo (uk.

73). Majoka kusema yuko katika safari ya jongomeo.

7iv. Kuonyesha udhaifu wa uongozi wa Sagamoyo. Majoka anamuuliza Daktari/Babu kama

ndiye rubani wa ombwe hilo (uk. 74)

v. Kujenga sifa za wahusika. Tunasawiriwa tama ya Husda inayomfanya kuuza pombe

haramu.

vi. Yanaangazia usaliti katiaka ndoa. Majoka anakiri kuwa anampenda Ashua; hampendi

mkewe Husda.

vii. Kuonyesha nafasi ya lmwanamke katika jamii; wanasawiriwa kama wasioweza

kutegemewa. Majoka anasema hawashikiki

viii. Kuonyesha ukosefu wa uwajibikaji wa uongozi. Majoka anasema hajashika usukani (uk.

80)ix. Kuonyehsa kuwa Wanasagamoyo wamezinduka. Majoka anasema wanaililia damu yake

(uk. 79)

x. Kuonyesha kwamba Sagamoyo haipigi hatua kimaendeleo. (uk. 81)

xi. Kuonyesha suala la mgongano kati ya utawala wa Babu na ule wa Majoka. Majoka

anasema kwamba athari ya chombo cha Babu/kinatikisa chake (cha Majoka) na

kukifanya kutaka kuubadilisha mkondo.

xii. Kutanabahisa/kumsuta Majoka kuhusu uongozi wake, na kumwonyesha haja ya

kubadilika. Babu anasema: Huoni kisima kimeingiwa paka na maji hayanyweki tena?

6. a)i. Akipanda harudi chini

ii. Hawezi kuporomoka /huanguka

iii. Amepta mbinu za kuendela kupanda (ameotesha makwezi)

iv. Makao/mahali pake ni pale juu/mamkani

v. Kushuka kwake si halali/ni haramu

vi. Hakumumiwa ila hubaki huko juu

vii. Haoni hatari wala wasiwasi

viii. Amejishikiza penye manufaa

ix. Amepanga mikakati ya kujipatia pato

x. Hata mti ukiporomoka, hushuki

xi. Hata akipigwa vita, hashuki

xii. Atakatalia juu hata akipigwa na radi

xiii. Hashuki kwa hiari

b) .i. Taswira hisi – ukweli jua mchungu/ yu furahani

ii. Taswira uoni – utabaki kutazama

iii. Taswira mguso – kugandama

8c) .i. Urudiaji silabi/ ngu, ngu, ngu (ubeti 1)

ii. Urudiaji wa neon – tangu, tangu amepanda akapanda

iii. Urudiaji wa mstari/kipande – mpanda ngazi jamani

d). i. Kufinyanga sarufi/kubananga lugha – hili mja ubaini – ubaini hili mja, mengi mazao –

mazao mengi

ii. Inkisari – ngawiraye – ngawira yake / walo – walio

e). i. Tanakuzi – mpanda – shuka, juu – ardhini

ii. Chuku – mpanda ngazi kubakia pale miaka na dahari/kushuka chini kuwa haramu

iii. Sitiari – mpanda ngazi – kiongozi anayepata mamlaka / kilelelkwenye mamlaka / ufanisi

f). i. Mistari mine katika ubeti

ii. Vipande viwili katika mishororo

iii. Vina vinabadilika kulingana na ubeti

iv. Mizaani 8,8 = 16 katika mshororo

v. Kipande cha mwisho cha ubeti kuanzia ubeti unaofuata

7 a) i. Alikuwa na uwezo wa kutenda mambo akiwa kijana, sasa hana

ii. Alikuwa na afya, sasa hana

iii. Alikuwa na ushirika wa ndugu na jamaa; sasa hana

iv. Anachoshika sic hake – sasa hamiliki lolote

v. Amepoteza baadhi ya viungo alivyokuwa navyo. Sasa hana neon

vi. Vitamu ni vichungu kwake

vii. Hana la kumfurahisha kama awali

viii. Vilivyokuwa laini vigumu

b). i. Shairi lina beti tatu

ii. Kila ubeti una mishororo saba

iii. Kila mshororo una vipande viwili

iv. Vina vya ndani na vya nje vinatiririka

v. Mizani 8,8 = 16 katika kila mshororo

vi. Kila ubeti unaanza kwa kauli; U wapi ujjana wangu

vii. Kila ubeti unajitosheleza

9viii. Kipande cha kwanza kinatoa wazo na cha pili kinakamilisha

ix. Shairi limetumia mistari kifu/toshelezi

x. Kila ubeti kuanza kwa swali la balagha

c).i. Taswira hisi – machungu

ii. Taswira uoni – tazama hii dunia

iii. Taswira mguso – laini , gumu

iv. Taswira muojo – kitamu, kichungu

v. Taswira mwendo – mayo imeshika njia

d). i. Kweli kinzani – kitamu sasa kichungu

ii. Tashhisi – afya imehsika njia

iii. Tasfida – wamehama ulimwengu

iv. Usambamba – Afya ya ujana wangu, siku ya ujanawangu.

e).i. Nafsineni – mzee/mtu aliyekonga

ii. Toni ya majuto/machungu kukata tama – U wapi ujana wangu?

8 a) Inaonyesha mwisho wa urafiki baina ya Sungura na Fisi-huo ukawa mwisho wa urafiki

wa Sungura na Fisi

b).i. Fanani kuzungumza moja kwa moja na h adhira – mjukuu wangu

ii. Matumizi ya chuki – mtu kujikwaa na mwingine kuwa ndiye anayehisi uchungu kuhitaji

kutwa kujaza tumbo

iii. Tashhisi – moyo wa fisi unamrai

iv. Methali – atanguliaye kisimani hunywa maji maenge

v. Nahau – alishika tariki

vi. Urudiaji – guu mosi, guu pili

vii. Ritifaa – sungura nazungumza na fisi na ilhali fisi hayupo

viii. Tasfida – uwezo wa kuyatoshelezea mumbile haja – badala ya – kwenda haja kubwa

ix. Kuigiza – alijikokota hivi…

x. Swali la balagha – itakuwaje…?

xi. Ucheshi – kicheko

xii. Tanakali za sauti – ndo ndo ndo!

xiii. Taswira – fisi akilia

xiv. Mtambaji kuhoji hali/ upenyezi wa mtambaji – sijui kama mjukuu wangu..

10.xv. Kuchanganya sauti ya usimulizi baina ya nafsi ya tatu hadi ya pili kupunguza masafa

ujumi kati ya fanani na hadhira

xvi. Kuchanganya nyakati (uliopita na sasa) ili kupunguza masafa ujumi.

c). i. Kuashiria mwisho wa usimulizi

ii. Kuiondoa hadhira kwenye ulimwengu wa fantasia hadi ulimwengu halisi

iii. Kuwapa kitulizo wasikilizaji/kuwaondolea watu mwemeo wa matukio ya hadithini

iv. Konyesha mwisho wa mgogoro wa hadithi ni – unaashiria mwisho wa urafiki wa fisi na

sungura

v. Kusawiri jamii ya fanani – ni wafugaji – anazungumza kuhusu ng’ombe

vi. Kuchochea wengine ili waweze kutamba hadithi

vii. Kusawiri mandhari ya jamii ya fanani

viii. Kuonyesha funzo la hadithi

d). i. Kushiriki kwa kupiga makofi

ii. Kushiriki kwa kuimba nyimbo,

iii. Kuigiza badhi ya matukio/matendo ya wahusika

iv. Kuuliza maswali

v. Kutoa mifano

vi. Hisia/wawazoonyesha usoni huweza kumfany abadilishe uwasilishaji

vii. Kuto-majibu kwa methali na vitendawili iwapo ngano itamalizikia kwa mtambaji

kuwategea vitendawili

viii. Kutoa mifano ya baadhi ya wahusika wa hadithini kutoa jamii zao iwapo wataulizwa

ix. Wanaweza kuchukua nafasi ya kuimba upya ngano hiyo

 

(Visited 235 times, 1 visits today)
Share this:

Written by