KCSE Past Papers 2020 Kiswahili Karatasi ya 1 (102/1)

Kenya Certificate of Secondary Education Kiswahili Karatasi ya 1 – Insha

Maagizo

Andika insha mbili. lnsha ya kwanza ni ya lazima.

Kisha chagua insha nyingine moja kati ya hizo tatu zilizobakia.

Kila insha isipungue maneno 400.

Kila insha ina alama 20.

Kila insha lazima iandikwe kwa lugha ya Kiswahili.

✤ Insha ya Lazima

1. Wewe ni katibu wa jopokazi ambalo limeteuliwa kuchunguza sababu za wanafunzi wa shule za upili kupuuza masomo ya kiufundi. Andika ripoti ya uchunguzi huo huku ukitoa mapendekezo.

✤ Chagua insha nyingine moja kati ya hizi tatu zilizobakia.

2. Maktaba ya shule yenu haina magazeti. Andika makala kuonyesha umuhimu wa maktaba hiyo kuwa na magazeti.

3. Tunga kisa kitakachodhihirisha maana ya methali ifuatayo:

✤ Mpanda ovyo hula ovyo.

4. Tunga kisa kinachoanza kwa maneno yafuatayo:

✤ Msongamano wa wanunuzi, wapitanjia na wasukuma mkokoteni katikati mwa wachuuzi wa kila aina ulinitanabahisha kuwa nimefika mji wa Tafaruku.

 

(Visited 460 times, 1 visits today)
Share this:

Written by