
Karatasi Ya 1 Insha Mwongozo Wa Kusahihisha
1. Hii ni ripoti
Yafuatayo yazingatiwe:-
a) Muundo
Sura ya ripoti idhihirike
i) Kichwa – kionyeshe kiini cha uchunguzi
ii) Utangulizi
- Mtahiniwa ataje jopokazi: wanachama walioteuliwa, aliyeteua jopokazi
- Hadidu za rejea (Masharti na mipaka ya utekelezaji wa kazi iliyopangiwajopokazi)
- Sampuli lengwa – habari zilikokusanywa
- Njia za ukusanyaji – hojaji, mahojiano, majadiliano kwenye vikundiiii) Mwili – Hoja zijadiliwe humu; vichwa vidogo vitumiwe
- Sababu/mapuuza/matokeo
- Mapendekezo
- Hitimisho
- Kimaliziob) Maudhui
Baadhi ya hoja ni:- i) Msisitizo mkubwa kwenye masomo ya kiakademia 2 ii) Kutokuwa na vielelezo tosha vy watu waliofanikiwa kwa kufuatia masomo ya aina hii iii) Masomo haya kutohimizwa katika shule nyingi kwa sababu ya ukosefu wa vifaa iv) Ukosefu wa walimu waliohitimu katika taaluma hizi v) Shinikizo kutoka kwa wazazi – wanafunzi wajishughulishe na masomo mengine vi) Mtazamo hasi kuwa baadhi ya masomo kama vile ufundi wa mabomba ni duni vii)Hapajawa na mfumo bayana unaoonyesha hatua ambazo mwanafunzi/mwanagenzi atapitia hadi pengine Chuo kikuu viii) Mafunzo mengine ya kiufundi ni ghali ix) Vyuo vichache vya kiufundi katika sehemu ya mashambani x) Vyuo vingine vya kiufundi vimegeuzwa kuwa vyuo vikuu, hivyo wanafunzi kutoona umuhimu wa vyuo vya kiufundi xi) Badhi huenda wasimudu masomo ya kisayansi, hivyo kukata tama xii)Masomo haya yanahitaji mtaji ndipo anayesomea apate ajira xiii) Mtazomo potovu uwa masomo haya ni ya mapato ya chini xiv) Walimu kuwavunja wanafunzi moyo xv) Masomo haya hayana mvuto kwa wanafunzi xvi) Masom haya huwafunga wanafunzi kukhusika wenyewe xvii) Mtazamo hari wa kijinsia kitamaduni, kitikadi xviii) Hoja zingine siko wazi c) Mahiniwa atoe angaa pendekezo moja kwa mafano i) Mtala usisitize masomo ya kiiufundi kuanzia ngazi za chini ii) Vyuo vya Ualimu vihusishe ufundishaji wa masomo ya kiufundi iii) Serikali iongezse ufadhili kwa masomo ya kiufundi iv) Kuwe na mfumo bayana unaoonyesha taaluma ambayo mwanafunzi atasomea akifuatia masomo ya kiufundi 2. Makala yaonyeshe umuhimu wa magazeti Sura ya Makala idhihirike Badhi ya hoja ni:- i) Kujuza kuhusu yanayojiri nchini/ulimwenguni ii) Kupalilia usomaji wa mapana iii) Kukuza ubunifu – mwanafunzi atajifunza mitindo mbalimbali ya uandishi iv) Kufunzia/kujifunzia sajili ya magazeti v) Baath hula an sofa yak kufunzia vipengele vya lugha vi) Hukuza stadi za kuhariri vii)Hupalilia uwazaji wa kina, kwa mfano kupitia kujaza mraba 3 viii) Kupalilia mazoea ya kusoma ix) Kufanikisha somo la maktaba x) Kupalilia mbinu za kitafiti/mazoea ya kudadisi xi) Kuburudisha xii)Kuimarisha masomo kupitia kwa maswali na majibu 3. Hii ni insha ya methali Kisha kidhihirishe maana ifuatayo Mtu asipotia bidii katika jambo matokeo yake huwa hafifu AU Kiasi cha kufanikiwa katika jambo hutegemea matayarisho/mikakati ambayo inawekwa Baadhi ya hali ambazo zinaweza kujitokeza ni:- i) Mwanafunzi kutojitayarisha ipasavyo kwa ajili ya mtihani na hatimaye kupata alama zisizoridhisha ii) Wakulima wakose kujiandaa ipasavyo, mwishowe wapate mavuno haba iii) Shirika likose kuweka mikakati ifaayo kuimarisha pato lake; lisipate faida, mwishowe lifilisike iv) Mlezi kutowaelekeza watoto ipasavyo, watoto kuinukia kuwa wasiotegemewa v) Mwajiri kutojaribu kuimarisha uhusiano wake na waajiriwa wake, migogoro izidi, uzalishaji mali uathirike vibaya Tanbihi 1. Vipengele vitatu vya kimuundo vijitokeze; utangulizi, mwili, hitimisho 2. Kichwa cha makala kidhihirike 3. Sharti insha idhihirishe juhudi hafifu/mikakati hafifu/ukosefu wa kujiandaa, na baadaye hali/matokeo yasiyoridhisha Hii ni insha ya kibunilizi Mtahiniwa atunge kisa ambacho kinaoana na mwanzo huu Usimulizi unaweza kubainisha hali zifuatazo i. Msimulizi asimulie yaliyotokea baada ya kuwasili, labda hata anaibiwa ii. Msimulizi aonyeshe alikoenda baada ya kuwasili, labda anapokelewa na mwenyeji wake; kasha asimulie maisha yake huko kwa mwenyeji wake iii. Anaweza kuwa anapitia hapa tu; pengine anatoka garini kupumzika kabla ya kuendelea na safari yake. Baadaye anaendeleza usimulizi wake hadi panapoishia safari iv. Msimulizi anaweza kuanza kwa kauli hizi, kasha ataturudhisha nyuma kusimulia kisa ambacho kinamleta hapa v. Anawea pia kusimulia maisha ya watu wa mji hu