KCSE Past Papers 2019 Kiswahili Karatasi ya 3 (102/3)

Kenya Certificate of Secondary Education Kiswahili – Fasihi Karatasi ya 3

SEHEMU A: RIWAYA

A. Matei: Chozi la Heri

1. Lazima

(a) “Sasa haya ameyapa kisogo … kufunguliwa kwa kituo hiki ni kama mana iliyomdondokea kinywani kutoka mbinguni.”

(i) Eleza muktadha wa dondoo hili. (alama 4)

(ii) Bainisha tamathali mbili za usemi ambazo zimetumiwa katika dondoo hili. (alama 2)

(iii) Fafanua umuhimu wa mhusika anayerejelewa katika dondoo hili katika kuijenga riwaya hii. (alama 6)

(b) Jadili mikakati mwafaka ambayo vijana wanatumia kukabiliana na hali yao ya maisha kwa kuwarejelea wahusika wafuatao:

(i) Chandachema (alama 4)

(ii) Dick (alama 4)

SEBEMU B: TAMTHILIA

P. Kea: Kigogo

Jibu swali la 2 au la 3

2. (a) Jadili mbinu kumi ambazo Wanasagamoyo wanatumia kupigana na utawala dhalimu. (alama 10)

(b) Eleza jinsi mbinu rejeshi ilivyotumiwa kukuza vipengele vifuatavyo katika tamthilia hii.

(i) Maudhui (alama 5)

(ii) Wahusika (alama 5)

3. (a) “Ushahidi utatoka wapi kama kipanga ndiye hakimu kwenye kesi ya kuku?”

(i) Eleza muktadha wa dondoo hili. (alama 4)

(ii) Fafanua dhima ya vipengele viwili vya kimtindo vinavyobainika katika dondoo hili. (alama 4)

(b) (i) Kwa kurejelea tamthilia jadili sifa sita za msemaji.(alama 6)

(ii) Eleza umuhimu wa mandhari katika tamthilia hii. (alama 6)

SEHEMU C: HADITHI FUPI

Jibu swali la 4 au la 5

A. Chokocho na D. Kayanda (Wah): Tumbo Lisiloshiha na Hadithi Nyingine

K. Walibora. “Nizikeni Papa Hapa”

4. (a) “Isije ikawa hapa habari ya kufuata asali ukafa mzingani.” “… Pana hasara gani nzi kufia kidondani?”

(i) Eleza muktadha wa dondoo hili. (alama 5)

(ii) Andika mbinu mbili za kimtindo zinazojitokeza katika dondoo hili. (alama 2)

(b) Hadithi, Nizikeni Papa Hapa inahimiza uwajibikaji. Jadili.(alama 5)

5. (a) Onyesha jinsi unafiki unavyoshughulikiwa katika hadithi, “Shogake Dada ana Ndevu.” (alama 8)

(b) Changanua mtindo katika dondoo lifuatalo: (alama 12)

“Bi. Hamida alitunga donge kifuani mwake. Na donge likaja juu. Likampanda na kumsakama kooni. Kweli? Uongo? Kweli au uongo yale maneno ya binti yake?

Labda kweli anamfıkiria mambo mabaya binti yake tu. Labda kweli dhana yake ni mbovu. Bi. Hamida alichanganyikiwa na mambo.

Alivutwa huku na huku na nafsi yake yenye chagizo. Upande mmoja sauti yake ya ndani ilikuwa inamtetea Safia, na upande wa pili wa nafsi yake ilikuwa ikimshuku Safia; na sauti zake zote mbili hizo zimo ndani ya kiwiliwili chake zinamvuta yeye mtu mmoja, Bi. Hamida. Hatimaye hakutambua afanye nini.”

SEHEMU D: USHAIRI

Jibu swali la 6 au la 7.

6.Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali

Lilipo lile banda, lile pale,
Kuna tuja kakonda, kwa uwele,
Wala siye kupenda, hiyo ndwele,
Ndwele ya kutishwa!

Ni ndwele ya kutengwa, penye haki,
Uwele wa kusutwa, pasi haki,
Ugonjwa kupuuzwa, na miliki,
Ndwele ya kutwishwa!

Mwiliwe kawa sugu,
viwandani, Uso una kunyugu,
ziso fani, Ujira wake ndugu,
ni mapeni, Ndwele ya kutwishwa!
Na homa akipatwa, maishani,
Kwa tiba apuuzwa, kama nyani,
Hajulikani kuwa, yeye nani,
Ndwele ya kutwishwa!

Ana chawa nyweleni, ona dhiki,
Na kunguni nguoni, ahiliki,
Funza na miguuni, wamesaki,
Ndwele ya kutwishwa!

Bado yuasubiri, kisimati, Dhiki yake kutiri, ‘we tamati Ndipo iwe sururi, ya kidhati Nyota yake ni nyota ya huzuni.

(K.Wamitila)

(a) Fafanua kwa kutoa hoja sita kutoka kwenye shairi, jinsi nyota ya anayerejele wa ni ya huzuni. (alama 6)

(b) Eleza muundo wa shairi hili. (alama 6)

(c) Bainisha aina zifuatazo za uhuru wa kishairi katika shairi: (alama 6)

(i) inkisari

(ii) kujifanyanga sarufi

(d) Eleza tamthali tutu za usemi zilizotumiwa katika shairi hili. (alama 3)

(f) Eleza sifa mbili za anayelengwa katika shairi hili kwa kurejelea ubeti wa mwisho. (alama 2)

(g) Andika ubeti wa nne kwa lugha nathari. (alama 2)

7. Soma Shairi lifuatalo kisha ujibu maswali.

Kalma akili si mali, maskini na tajiri
Wangalimoja sampuli, asikuwepo fakiri
Na hangekuwa na mali, mwinyi bila kufikiri
Kama akİlİ si mali, usingeweza fikiri.

Ukeshapo kwa fikara, ni kwa wingi wa akili
Kuwaza kigaragara, una mengi si kalili
Na kuwa una tambara, metajirika kwa hili
Kama akili si mali, usingeweza fikiri.
Alokijenga kitanda, ana wingi wa akili
Hata asiwe na bunda, hamithili kwa akili
Hata naye paka nunda, pasipo akili hali
Kama akili si mali, usingeweza fikiri.

Akili kweli ni mali, kwa kuteua vya mwozo
Singetumia akili, ungevila vya angamizo
Afya ikawa thakili, na kuhiliki mawazo
Kama akili si mali, usingeweza fikiri.

Vipi gonjwa kikuganda, wawazia spitali?
Huachi ukawa ng’onda, ukanyauka muwili
Ugangani unakwenda, kutafuta afadhali,
Kama akili si mali, usingeweza fikiri.

Kama akili si mali, kusingekuwa na jela,
Kuwatenga kuwa mbali, wenye hiana na hila,
Kwa mbavu na ufidhuli, pamwe mbinu tolatola,
Kama akili si mali, usingeweza fikiri.

Tajiri na maskini wote wanayo akili,
Ni kuwa hayafanani, waliyonayo makali
Kabisa hawashibani, liwe lile au hili,
Kama akili si mali, usingeweza fikiri.

Kalma akili si mali, ‘singekuwa na hazina
Ya kudadisi mithali, na kumpinga yako mnna
Gani inadumu mali, kuliko huko kusana?
Kama akili si mali, usingeweza fikiri.

(T. Arege)

(a) “Ufanisi wa binadamu hutegemea akili.” Fafanua kwa kurejelea hoja sita kutoka kwenye shairi hili. (alama 6)

(b) Andika mifano ya vipengele vifuatavyo vya kimtindo katika shairi hili:(alama 4)

(i) sitiari

(ii) tanakuzi

(iii) Swali la balagha

(iv) kinaya

(c) Eleza mbinu nne ambazo mshairi ametumia kutosheleza mahitaji ya kiarudhi. (alama 4)

(d) Andika aina mbili za urudiaji zinazojitokeza katika shairi hili.(alama 2)

(e) Fafanua muundo wa shairi hili.(alama 4)

SEHEMU E: FASIHI SIMULIZI

8. Soma utungo ufuatao kisha ujibu maswali. Shangazi anambila
umewadia muda
wa kukiacha kiambo
cha Baba
Nende kujinasibisha
na ajinabi tusohusiana
kwa ngeu wala usaha
nache niwapendao
nache aila
nache matamanio
ya elimu kufuatiya.

Anambile shangazi
Hino ni neema
ela moyo wanirai
“Wajitia shemere”, nami nauambia,
“Najua si utashi wangu”
ila hiari sina

kwani lvii ni faradhi
mitamba mepokelewa
na ami kwa furaha
kilobaki ni kuvuka
kizingiti hiki.”
Kwaheri’i Mama, kwaheri wanuna.

(a) Ainisha wimbo huu kwa kuzingatia kipengele cha maudhui.(alama 2)

(b) Andika sifa mbili za jamii inayosawiriwa na wimbo huu. (alama 2)

(d) Unanuia kutumia mahojiano kukusanya habari kuhusu nyimbo za aina hii.

(i) Eleza manufaa matano ya kutumia mbinu hii.(alama 5)

(ii) Eleza changamoto tano za kutumia mbinu hii.(alama 5)

 

(Visited 337 times, 1 visits today)
Share this:

Written by