KCSE Past Papers 2017 Kiswahili Paper 2 (102/2)

2017 Kiswahili Karatasi ya 2

Lugha

Ufahamu Maswali na Majibu: (Alama 15)

(a) “Kufauikiwa kwa watu wenye mahitaji maalumu ktmategemea jamii.” Thibitisha kwa kutoa hoja sita kutoka aya tatu za kwanza. (alama 6)

  • Wazazi Wanampeleka Bahati shuleni.
  • Bahati kupata dhiki ya kisaikolojia kwa kudhihakiwa
  • Wazazi kumtafutiaB ahati mlinzi wa kumkinga na wateka nyara.
  • Bahati na wengine kama yeye kusoma hati za kawaida hapo awali
  • Bahati kubaguliwa kazini
  • Serikali kuhakikisha matini zimeandikwa kwa hati inayoweza kusomwa na Walemavu
  • Wazazi hawamfunzi Bahati mbinu za kujilinda, hivyo anajihisi mfungwa.
  • Walanguzi Wa Watu kuhatarisha usalama wa watoto wa aina ya Bahati
  • Ukoo kuamua kuangamiza watoto wenye ulemavu
  • Bahati kudhihakiwa shuleni/kutengwa na Wenzake
  • Mama/wazazi kuamua kumhifadhi Bahati Tanbihi Mtahiniwa anaweza kuangazia dhuluma pekec. Anaweza pia kuangazia utekelezaji wa haki kwa Watu Wenye mahitaji maalumu pekee. Anaweza pia kuchanganya hoja. Mradi amedondoa hoja sita. ((b) Kwa kurejelea aya ya nne hadi ya saba, onyesha jinsi unyanyasaji Wa kijinsia unavyoendelezwa katika jamii hii. (alama 3)

    (i). Muuguzi kutalikiwa kwa kutopata mtoto

    (ii). Watoto Wa kike kuonekana kuwa mzigo/si Watoto

    (iii). Kusimangwa na mavyzia — kuwa hajazaa Watoto.

    (c) “Msimulizi anahimiza. uwajibikaji.” Thibitisha kwa kutoa hoja nne kutoka aya tatu za ‘ mwisho. (alama 4)

     

  • Mume kuondoka bila neno kwa mkewe ~ anakuja kuomba msamaha.
  • hisia za mama/wazazi
  • Mume kumjuza mke uamuzi wa ukoo
  • Mume kulipia gharama ya matibabu
  • Msimulizi kuamua kukihifadhi kitoto chake
  • Msimulizi anakashifu mtazamo Wa jamii kuhusu watoto wa aina hii. (aya ya mwisho) ‘ Tanbihi Mtahiniwa anaweza kuonyesha uwajibikaji au hata ukosefu Wa uwajibikaji. Anaweza kuchanganya hoja pia.(d) (i) Andika kisawe cha, ‘hisani’ kwa mujibu wa taarifa. (alama 1)

     

  • Hisani- fadhila, shukrani (alama 1)(ii) Eleza maana ya, ‘kuupaka masizi’ kulingana na taarifa. (alama 1)

     

  • Kuupaka masizi — kuuharibia sifa/ kuuaibisha2. Ufupisho Maswali na Majibu: (Alama 15)

    (a) Fupisha ujumbe wa aya nne za kwanza kwa maneno 90. (alama 8, 1 ya mtiririko) Matayarisho

    Sayansi na teknolojia zimerahisisha maisha ya binadamu.

  • Mashine zimerahisisha utenda kazi.
  • Mtu anaweza kusomesha hata bila kuwepo.
  • Kuimarisha shughuli za utafiti
  • Kurahisisha usajili Wa wanafunzi na watahiniwa vii. Kuimarisha matibabu kupitia utafiti
  • Kufanya udososi hapo hapo
  • Kurahisisha ubadilishanaji bidhaa
  • Kuhifadhi na kutuma pesa
  • Kulipia huduma(b) Fafanua masuala ambayo mwandishi anaibua katika aya tatu za mwisho. (maneno 70) (alama 7, 1 ya mtiririko) Nakalasafi

    .

  • Nafasi ya uvumbuzi wa kisayansi
  • Kuzorotesha utenda kazi
  • Kuingilia uhuru Wa kibinafsi
  • Kuwatisha wengine
  • Kuwamsi na kuwadhalilisha wengine
  • Kuwatapeli vii. Wizi Wa kitaaluma vm. Upujufu Wa thamani ya n1tihani/ Wizi Wa mitihani
  • Visa vya kigaidi kuendelezwa kupitia mtandao
  • Kumomonyoa mshikamano wa kifamilia- mawasiliano ya sirnu badala ya ana kwa ana
  • Vijana kupuuza masomo kwa kuwa Waraibu wa mtandao
  • Binadamu huweza kupata mafundisho ya kidini kupitia mtandao.
  • Kupalilia ukosefu wa ajira
  • Binadamu atumie teknolojia kwa njia endelevu ili kujifaidi.3. MATUMIZI YA LUGHA: (Alama 40)

    (a) Andika tofauti moja kati ya sauti zifuatazo: (alama 2)

    (i) /ng’/na/gh/– /ng’/ni nazali na /gh/ni kikwamizo

    (ii) /v/ na /f/– /v/ ni ghuna na /f/ sighuna.

    (iii) /r/na/l/– /r/ ni kimadende na /l/ ni kitarnbaza.

    (iv) /m/na/n/– /m/ hutamkiwa midomoni i1hali/n/ ni ya ufizi.

    (b) Andika.

    (i) konsonanti, konsonanti, konsonanti, irabu, konsonanti, irabu

    mfano:mbweha, ngwena, ndwele

    (ii)konsonanti, konsonanti, irabu, konsonanti, irabu

    mfano:ndama, mkate, ngama, ndizi, mkeka

    (c) Tunga sentensi mbili kuonyesha matumizi mbili ya kiambishi O

     

  • Kirej eshi cha nafsi ya tatu wingi — Wafanyakazi walioajiriwa wana bidii. 
  • Kirejeshi cha ngeli ya U — I — Umoja Mgiu uliotibiwa umepona.
  • Kirejeshi cha ngeli ya U — ZI — umoja Ufa uliozibwa ni huu,
  • Kirejeshi cha ngeli ya U — YA — umoja Ugonjwa huu ndio uliotibiwa.
  • Kirejcshi cha ngeli ya U — U — Wema aliomonyesha ulituvutia.
  • Kuonyesha tokeo la kitu/kuonyesha nomino/unominishaji(d) Andika sentensi zifuatazo upya kulingana na maagizo. (alama‘2)

    (i) Mhalifu alisamehewa kwa sababu alinyenyekea.

    (Geuza maneno yaliyopigiwa mstari kuwa nomino.)

    – Mhalifu alipata (alipewa) msamaha kwa sababu (kwa) unyenyekevu wake.

    (ii) Waigizaji wengine wameingia jukwaani.

    (Tumia kivumishi cha idadi chenye kuonyesha nafasi katika orodha.)

    – Waigizaji wa kwanza/wa mwisho wameingia ju.kwaani

    (e) Tunga sentensi ukitumia kirai kihusishi kama kielezi.

    (i)Mama huyo aliwapenda wanawe kwa dhati.

    ii. Bendera ilikuwa juu ya mlingoti.

    (iii). Mkurugenzi aliwasili kabla ya mkutano kuanza.

    iv. Kaire ni mrefu kuliko baba yake.

    (f) Unganisha sentensi zifuatazo kwa viunganishi mwafaka.

    (i) Kheri aliweza kutujengea hospitali. Atajenga zahanati pia.

    – Kheri aliweza kutujengea hospitali sembuse zahanati!

    (ii) Zumari anasomea unasheria vile vile Maki anasomea unasheria

    – Zumari na Maki wanasomea Uanasheria.

    (g) Onyesha miundo ya nomino kafiika ngeli ya A — WA.

    Nomino zinazoanza kwa ‘m’ katika umoja na ‘Wa’ katika wingi. Mfano: Mbunge ~ Wabunge

    ii. Zinazoanza kwa mw katika umoja na wa katika wingi.

    Mfano Mwanasheria ~ Wanasheria j n m. Nomino za pekee zinazotaja watu. Maria ametutembelea.

    iv. Zinazoanza kwa’ki’ katika umoja na‘vy’ katika wingi

    a) Kijana huyu ameheshimika. Vijana hawa wameheshimika.

    b) Kiboko angalimajini. Viboko wangali majini.

    v. Ambazo hazina mianzo maalum ila huchukua viambishi A — WA vya upatanisho wa kisarufi.

    Kwa mfano, simba, kuku, bata, mama, baba. Simba huyu amehifadhiwa. Simba hawa wamehifadhiwa.

    (h) Tunga sentensi katika wakati uliopo hali isiyodhihirika.

    (i) Wanariadha Wacheza uwanj ani.

    ii. Jua lachomoza asubuhi.

    iii. Sisi twasoma vitabu.

    iv. Mwalimu afundisha darasani.

    (i) Andika sentensi ifuatayo katika umoja.

    ‘ Maseremala walilainisha mbao hizo wakatutengenezea meza.

    – Seremala alilainisha ubao huo akanitengenezea meza.

    (j) Andika upya sentensi zifuatazo kulingana na maagizo.

    . (i) Kaumu amewafanya mifugo wangu wanywe maji.

    (Anza kwa: Mifugo wangu , usitumie, ‘amewafanya’.) Mifugo wangu wamenyweshwa maji na Kaumu.

    (ii) Wanakijiji wanaishi karibu na msitu. Wanakijiji hawawavamii wanyama.

    (Ungamsha kuunda sentensi ambatano.)

    Wanakijiji wanaishi karibu na misitu lakini|ila|bali|i1hali hawawavamii wanyama

    (k) Andika sentensi ifuatayo katika hali ya ukubwa.

    Ngoma hizo zao ziliibwa na wezi Wale.

    Magoma hayo yao yaliibwa na majizi yale.

    (I)Tumia ‘kwa’ katika sentensi kuonyesha:

    (i) schemu ya kitu kizima (alama 1)

    Watoto Watatu kwa kumi hupata chanjo hiyo

    (ii) namna tendo lilivyofanyika (alama 1)

    Wengine walipata tisa kwa kumi katika tamrini hiyo. Andika sentensi ifuatayo katika usemi wa taarifa. (alama 2)

    “Kusoma kwa mapana kutapalilia ubunifu wa wanafunzi hawa wenu,” mtaalamu akatuambia.

    – Mtaalamu alituambia kwamba kusoma kwa mapana kungepalilia ubunifu wa wanafunzi haowetu

    Ainisha vishazi katika sentensi ifuatayo. (alama 2)

    Viwanda vikianzishwa masharnbani idadi ya wanaohamia mjini itapunguzwa.

    (i)Viwanda vikianzishwa mashambani — kishazi kitegemezi

    (ii) Idadi ya wanaohamia jijini- kishazi kitegemezi

    (iii) Itapunguzwa — kishazi huru

    Tunga sentensi zenye miundo ifuatayo. (alama 2′)

    (i) KN(N+RH)+KT(Ts+’l’)

    – Umati wa Watu ulikuwa ukimshangilia.

    – Kisu cha baba kinahitaji kunolewa

    (ii) KN(V+N)+KT (t+v)

    – Mwenye duka angali mwaminifu. b) Yule dalali alikuwa shupavu

    Ainisha yambwa katika sentensi ifuatayo.

    Mhunzi alimfulia mjukuu wake pete ya shaba. (alama I)

    Mjukuu wake — yambwa tendewa (kitondo) Pete ya shaba – yambwa tendwa (kipozi) Tanbihi

    Bainisha maana mbili zinazojitokeza katika sentensi ifuatayo.

    Bedui alimrushia tufe.

    (i)Alirusha tufe kwa niaba ya mhusika huyo.

    (ii) Alirusha tufe kuelekea kwa mhusika huyo.

    (iii) Alirusha tufe ya mhusika huyo.

    (iv) Alimrusha mhusika huyo kwa sababu ya tufe.

    Alama za mtajo hutumiwa kufungia maneno halisi ya msemaji. Tunga sentensi moja kuonyesha matumizi mengine mawili ya alama za mtajo.

    (i)Kufungia neno la kigeni- “mukimo”

    (ii) Kuonyesha neno lina maana nyingine na unayomaanisha, k.m. binamu kumaanisha ‘mpenzi’.

    (iii) Kufungia anwani- “Pendo la Karaha”

    (iv) Kuonyesha neno halij akubaliwa katika lugha unayoandikia/unayoziingumza.

    (s) Andika sentensi ifuatayo upya kwa kutumia kinyume cha maneno yaliyopigiwa mstari Mwanafunzi mkakamavu huzingatia masomo yake.

    – Mkakamavu — mzembe/mvivu/mnyonge/goigoi/Intepetevu/dhaifu huzingatia masomo yake

    (t) Tunga sentensi moja kutofautisha maana ya rithi na ridhi.

    – Rithi — kupata mali/maarifa au ujuzi kutoka kwa mtu/makala fulani Ridhi — kukubali au kupendezwa na jambo/kutoa ruhusa jambo litendeke.

    (u) Tunatumia simile tunapotaka mtu atupishe, hamadi..tunapoomba kitu kinusurike, na kefule……..tunapoudhika. …tunapokasirishwa……….na jambo,

    (v) Andika visawe vya maneno yafuatayo:

    (i) doa

    – dosari, kosa, hitilafu, ila, baka

    (ii)omba — rai, sihi, sali

    (w) Andika sentensi ifuatayo upya kulingana na maagizo.

    Maneo haya yana uyoga

    (Anza kwa: Uyoga.)

    (i) Uyoga hupatikana kwenye maeneo haya.

    ii) Uyoga hupatikana katika maeneo haya.

    iii) Uyoga upo kwenye maeneo haya.

    4. ISIMUJAMII: (Alama 10)

    Soma makala yafizatayo kisha ujibu maswali.

    “Kwa mujibu wa ushahidi uliotolewa, mahakama hii irnethibitisha bila chembe ya shaka kwamba wewe mshtakiwa, Bi Mlachake Chauchau ndiye uliyepika pombe haramu ambayo ilisababisha vifo vya raia harnsini na kupofuka kwa wengine mia moja. Unahukumiwa kwa kosa la mauaji.”

    (a) Bainisha sajili ya makala haya kwa kutoa rnifano miwili kutoka kwenyc makala.

    – Sajili ya mahakamani/sajili ya kisheria

    i) Matumizi ya sentensi ndefu – sentensi ya kwanza inatakriban maneno 30.

    (ii) Msamiati maalum Wa kisheria kama vile ‘ushahidi’,‘mahakama’,‘unahukumiWa’

    (iii) Kuzungumza na mshukiwa moja kwa m0ja- wewe mshukiwa

    (iv) Kutoa hukumu

    (b) Fafanua sifa nyingine nane za sajili hii ambazo zingejitokeza katika makala haya. (alama 8)

    (i) Matumizi ya lugha chakavu/kikale

    (ii) Kunukuu vifungu vya sheria ili kuondoa shaka.

    (v) Kuzingatia urasmi kwa kiasi kikubwa

    (vi) Urudiaji unaonuiwa kuweka wazo wazi/kusisitiza

    (vii) Msamiati Wa kawaida hupcwa/huwa na maana maalum. Kwa mfano unaposema, “Leamed Friend”, kurnaanisha mwanasheria.

    (viii) Lugha ya kuhoji/kudadisi, hasa pale mshukiwa/shahidi anapohojiwa.

    (ix) Sheria za kisarufi huzingatiwa kwa kiasi kikubwa ili kukinga dhidi ya kupotosha maana.

    (X)

    (xi) Kauli fupifupi hasa wakati wa kuhoji.

    (xii) Upashanaji zamu kwa kawaida hudhibitiwa na kiongozi wa mashtaka.

    (xiii) Kuchanganya

    (xiv) Lugha ya kushawishi, hasa pale wakili anapotoa utetezi

    (xv) Toni kali pale hakimu anapotoa hukumu. Wakati mwingine sheria hizi huweza kuvunjwa ili kukidhi haja ya mawasiliano, hasa pale mshukiwa hajasoma/haelewi lugha rasmi au lugha sanifu.

  •  au kubadilisha msimbo huweza kutokea.
(Visited 756 times, 1 visits today)
Share this:

Written by