KCSE Past Papers 2015 Kiswahili Paper 3 (102/3)

Karatasi ya 3

FASIHI

SEHEMU A : FASIHI SIMULIZI

Lazima

(a) Soma utungo ufilatao kisha ujibu maswali.

Hadithi ya Jabari inasimuliwa na jamii nyingi. Jabari alizaliwa kashika mkuki mkononi. Mawio ambayo kilio chakc, ambacho kwa kweli kilikuwa mugurumo, kilipopasua anga, nyota kubwa ilianguka kutoka mbinguni. Ulimwengu mzima ulitetemeka na kutwaa giza.

Hata kabla mama mtu hajampa ziwa, Jabari alikuwa amevuvumuka ua kuwa ghulamu wa miraba minne. Haikuchukua muda, hata vita kati ya jamii ya Sule na Suna vikaanza; kikosi cha Sule cha wapiganaji mia moja kikawajia vijana wa Suna kwa sime na nyuta. Jabari aliwakabili kwa konde moja pekee, akakirambisha dongo kita kizima

(i)Bainisha kipera cha utungo huu. (alama 1)

……………………..

(ii)Toa sababu mbili kuthibitisha jibu lako la (i)hapa juu. + (alama 1)

……………………..

(iii)Eleza manufaa sita ambayo jamii itapata kwa kukirithisha kipera hiki kwa vizazi vijavyo. (alama 6)

……………………..

(b) Soma utungo ufuatao kisha ujibu maswali.

Ndimi Mwimo mdumishaji ukoo

Ndimi ndovu mtetemesha ardhi

Aliyegigang vita, ukoo kuauni

Ziliporindima zangu nyayo

édui alinywea, mafahali na mitamba akatukabidhi

Kwenye misitu sikuwa na kifani

Paa na hata visungura

vilijikabidhi kwangu

kwa kuinusa tu mata

Nani aliyewahi

ngomani kunipiku?

Makoo hawakunisifu, wakalilia nikaha?

Kwenye nyanja za michuano

nani angethubutu, ndaro kunipigia?

Sikuwabwaga chini, kwa yangu maozi, hata kabla hatujavaana?

(i) Andika aina ya sifo hii. (alama 1)

………………………

(ii) Bainisha shughuli mbili za kiuchumi na mbili za kijamii zinazoendelezwa na jamii inayosawiriwa na utungo huu.(alama 2)

………………………

(iii) Eleza mambo matano ambayo yanaweza kuzingatiwa ili kufanikisha uwasilishaji wa mungo huu .(alama 5)

………………………

(c) Eleza faida nne za matumizi ya nyimbo katika uwasilishaji wa ngano. (alama 4)

………………………

SEIIEMU B: RIWAYA

K. Wllibora: Kidagaa Kimemwozea

Jibu swali la 2 au la 3.

2. “Moyo ulimpapa na kijasho chcmbamba kumtekenya juu ya mwanzi wa pua. Akahisi uchungu wa mwiba wa kujidunga.”

(a) Eleza muktadha wa dondoo hili. (alama 4)

……………………

(b) Huku ukirejelea riwaya hii, fafanua kwa kutoa hoja nane, namna anayelengwa na kauli hii alivyojidunga miiba. (alama 16)

…………………………..

3. (a) “Imani ni kielelezo cha vijana waliowajibika.” Thibitisha kauli hii kwa kurejelea mifano kumi kutoka Kidagaa Kimemwozea. (alama 10)

…………………………..

(b) “Nadhani Mzungu pale alipo hana budi kutambua ukomavu Wa Mwafiika katika kila sekta ya maisha

Onyesha kinyume katika kauli iliyopigiwa mstari kwa kurejelea uongozi wa Tomoko (alama 10)

…………………………..

SEHEMU C: TAMTHILIA

T. Arege: Mstahiki Meya

Jibu swali la 4 au la 5. 4. “Kushindana naye ni kama kushindana na ndovu. Utapasuka”

(a) (i) Eleza muktadha wa dondoo hili.(alama 4)p> …………………………..

(ii) Bainisha tamathali moja ya usemi inayojitokeza katika dondoo hill.(alama 2)

…………………………..

(b) Kwa kurejelea hoja saba, thibitisha kwamba kushindana na anayerejelewa na kauli hii ni sawa na kushindana na ndovu.(alama 14)

…………………………..

5. “Wahenga wanasema dawa ya adui ni kummegea unachokula.” (a) (i) Andika suala linalodokezwa na kauli iliyopigiwa mstari.(alama 2)

……………………….

(ii) Jadili hoja nane zinazoonyesha namna suala hili linavyozorotcsha hali ya maisha Cheneo.(alama 8)

………………………

(b) Jadili jinsi vyombo vya usalama vilivyotumiwa kuuendeleza uongozi wa Cheneo.(alama 10)

……………………..

SEHEMU D: USHAIRI

Jibu swali la 6 au la 7. 6.Soma shairi Iifuatalo kisha ujibu maswali.

Daima alfajiri na mapema

Hunipitia na jembe na kotama

Katika njia iendayo kondeni

Kama walivyofanya babuze zamani;

Nimuonapo huwa anatabasamu

Kama mtu aliye na kubwa hamu

Kushika mpini na kutokwa jasho

Ili kujikimu kupata malisho.

 

Anapotembea anasikiliza

Vidcge vya anga vinavyotumbuiza

Utadhani huwa vimemngojea

Kwa usiku kucha kuja kumwimbia;

Pia pepo baridi kumpepea

Rihvi ya maua zikimletea

Nao umande kumbusu miguu;

Na miti yote hujipinda migongo

kumpapasa, kumtoamatongo;

Na yeye kuendelea kwa furaha

kuliko yeyote ninayemjua

Akichekelea ha ha ha ha ha ha

 

Na mimi kubaki kujiuliza

Kuna siri gani inayomliwaza?

Au ni kujua au kutojua?

F uraha ya mtu ni furaha gani

katika dunia inayomhini?

Ukali wa jua wamnyima zao

Soko la dunia lamkaba koo;

Dini za kudhani zamsonga roho

Ayalimia matumbo ya waroho;

Kuna jambo gani linamridhisha?

Kama si kujua ni kutokujua

Laiti angalijua, laiti angalijua!

(T. Arege)

(a) Eleza hali ya mzungumziwa katika shairi hili. (alama 4)

……………………..

(b) Huku ukitoa mifano, onyesha aina mbili za uhuru wa kishairi uliotumiwa katika shairi hili.(alama 2)

……………………..

(c) Fafanua aina tatu za taswira ukirejelea ubeti wa pili.(alama 3)

…………………..

(d) Eleza umuhimu wa maswali ya balagha katika shairi hili.(alama 2)

…………………

(e) Bainisha vipengele vifuatavyo vya kimtindo katika shairi hili:(alarna 3)

(i) tashhisi

………………………

(ii) kinaya

………………………

(iii) tashbihi

……………………….

(f) Eleza toni ya shairi hili.(alama 2)

………………………

(g) Bainisha nafsineni katika shairi hili.(alama 1)

………………..

(h) Changanua muundo wa shairi hili.(alama 3)

……………………….

7.Soma Shairi lifixatalo kisha ujibu maswali.

T. Arege: Mwili

Leo kitaka nifike, natamani, ila wauma mwili

Kwa kazi nihusike, samahani, unahiliki mwili

Napenda nihesabike, makundini, ila huwezi mwili.

 

Vitisho amw kelele ninavicha, kwa nafsi na mwili

I1a , umechacha, na kuudhili mwili

Msikose simile, magalacha, si gurudumu mwili.

 

Vingekuwepo viraka, kuutia, ngeushuruti mwili

Kifundi kivipachika, kuingia, hata kuridhi mwili

Upya ukaungilika, kuvutia, roho na wake mwili.

 

Lakini kamwe haiwi, kuvipata, vipande vyake mwili

Sihofu kupata mawi, sitajuta, kupigania mwili

Hata kufutwa sikawi, nitakita, kidete nao mwili.

 

Kazi ninaithamini, ni hakika, akilini na mwili

Ila kamwe siamini, kusagika, damu, jasho na mwili

Uwele hususani kioheka, nguvu hitishi mwili.

(a) Eleza dhamira ya mtunzi wa shairi‘hi1i. (alama 4)

……………………..

(b) Fafanua mbinu nneza lugha zilizotumiwa katika shairi hili. (alama 8)

……………………..

(c) Eleza toni ya shairi hili.(alama 2)

………………………

(d) Ni nani anayezungumziwa na nafsineni katika shairi hili? (alama 1) (e) Eleza bahari ya shairi hili kwa kurejelea vipande. (alama 2)

……………………….

(f) Andika ubeti wa mwisho kwa lugha ya nathari. (alama 3)

………………….

SEHEMU E: HADITHI FUPI

K. Walibora na S. A. Mohamed (Wah) : Damu Nyeusi na Hadithi Nyingine

“Mizizi na Matawi” (A. Abdulla Ali)

8. (a) “Mwisho, naomba sote tusameheane kwa dhati.”

(i) Fafanua muktadha Wa dondoo hili. (alama 4)

………………………..

(ii) Jadili umuhimu wa hotuba ya mzungumzaji katika hadithi hii. (alama 8)

…………………………..

(b) Onyesha jinsi hadithi, “Mke wangu” ilivyotumia kinaya kufanikisha ujumbe Wake. (alama 8)

…………………………..

 

(Visited 893 times, 1 visits today)
Share this:

Written by